MSANII KUTOKA AFRIKA KCEE WA NIGERIA, AFANYA COLLABO NA NICKI MINAJ, KWA KUMLIPA MWANADADA HUYO TSH MIL 675

STREETCONSCIOUS.BLOG

kcee-and-Nicki-Minaj
Kama ulishangaa kusikia kuwa Diamond Platnumz alilipa dola 5,000 ili kumshirikisha Davido kwenye remix ya My Number One, huenda ukaishiwa nguvu kusikia kiwango kinachodaiwa kutolewa na msanii wa Nigeria, KCEE ili kufanya collabo na first lady wa YMCMB, Nicki Minaj.
posts_78640479381
Kuna tetesi kuwa KCEE amelipa kitita cha N68m, ambazo ni zaidi ya shilingi milioni 675 za Tanzania ili amshirikishe malkia huyo wa hip hop nchini Marekani. Kufuatia tetesi hiyo, meneja wa KCEE, Soso Sobrekon, ameongea na mtandao wa NET kufafanua mambo yalivyo.
“Tupo nchini Marekani kujaribu kupata collaboration. Ni kweli tupo kwenye mchakato wa kufanya wimbo na Nicki Minaj. Tulitaka kuifanya iwe surprise kwa mashabiki lakini kwakuwa tayari imejulikana, tunataka kuifanya iwe kuwa zaidi,” alisema.
playboy-nicki-minaj-639437
Hata hivyo meneja huyo alikataa kuthibitisha kama kweli kiwango hicho ndicho walicholipa. “Tunataka kumuongeza msanii mwingine wa YMCMB ambaye ni mkubwa kuliko Nicki Minaj. Nicki ameshathibitishwa kuwa kwenye wimbo huo, lakini kwakuwa sasa kila mtu anafahamu, bado tutawasurprise mashabiki kwa kumchukua msanii mwingine kutoka YMCMB.’
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment