Dr Dre Ameifuta record ya Forbes iliyowekwa na P Diddy mwaka huu. Kama
unakumbuka Forbes ilitoa list ya wasanii wa hiphop watano walio na
mkwanja, ambapo Dre alikuwa nafasi ya pili kwa kuwa na dola milioni 550
ambapo Didiy alikuwa anaongoza kwa kuwa na dola milioni 700.
Kwa mujibu wa habari zilizotoka leo hii, kampuni ya Apple inampango wa
kuinunua kampuni ya Dre Beats Electronics kwa dola bilioni 3.2. Kampuni
hiyo ilianzishwa na Dre pamoja na Jimmy mwaka 2008 kwa kutengeneza vifaa
vya sauti kama headphones, speaker za magari pamoja na mtandao wa ku
stream muziki.
Baada ya maneno kusambaa kuwa kampuni ya Apple iko mwishoni kukamilisha
mkataba huo, Dre alienda studio akiwa na Tyrese, F Gary Gray (Big time
movie director) na baadhi ya washkaji nakusherehekea kwa chupa za
Champagne, Heineken na Henennessy.
katika video waliji-record Dre ameonekana akiangalia camera na kusema
"Bilionea wa kwanza katika game ya hip hop, kutoka west coast.
huku Tyrese akisema "oooh sh""t list ya Forbes imebadilika

0 comments:
Post a Comment