Janjaro awataja Madee, Tundaman na Babu Tale kwenye wimbo wake 'Fungua Macho' aliofanya B'Hitz

Dogo Janja aka Janjaro ambaye alitambulishwa na Madee wa Tip Top Connection kwenye game la Bongo Flava na kujizolea mashabiki wengi kwa uwezo wake mkubwa wa kurap, na baadae kuondolewa kwenye familia ya Tip Top kutokana na tofauti zilizojitokeza, anatarajia kuachia wimbo mpya alioupa jina la ‘Fungua Macho’ ambapo ndani amewataja Madee, Tundaman na Babu Tale.
Janjaro ameiambia HOT SHOW kuwa anatarajia kuachia wimbo huo alioufanya ndani ya studio za B’Hitz chini ya producer Pancho Latino na kwamba humo ndani ameonesha upendo kwa Madee na Tundaman, pamoja na Boss wao Babu Tale, amewaomba wasahau ya kale kwa kuwa yeye sio Nabii.
Janjaro aliipa HOT SHOW ya HIGHLANDS Fm sehemu ya mashairi yaliyopo kwenye ngoma hiyo.
“Bado niko macho nasukuma gurudumu, nashukuru nikipatacho kinacover majukumu. Tusahau ya kale Tunda msalime Madee, mwambie Babu Tale Janjaro sio Nabii…”
Janjaro ameielezea kwa ufupi mistari hiyo, “vitu kama hivyo vinaleta upendo katika wimbo. Unajua kitu kama Tip Top ni watu ambao mimi wamenilea, kwa hiyo Janjaro sio nabii, hata glass hugongana…kunatokea matatizo lakini tusahau ya kale.”
Ameeleza kuwa hivi sasa uhusiano wake na Madee umeimarika na wanaongea vizuri. Amewashukuru watanzania kwa upendo wanaomuonesha.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment