![]() |
| AZMA THE AFRICAN AMBASSADOR |
Ni wasanii wachache wa Hip Hop Africa mashariki pengine
na afrika nzima kwa ujumla waliowahi kutoa na kupeleka sokoni album zao zenye
video tupu, uchache huo pengine unatokana na kutokuwa na mda wa kutosha kuandaa
album yenye video tupu ama kutomudu gharama za kifedha kufanya video.
Azma a.k.a the African ambassador hit maker wa
Kipimo cha penzi, Wanasuburi nife na Mungu inusuru Tanzania atakuwa msanii wa
kwanza wa Hip Hop nchini Tanzania kutoa album yenye video tupu.
Akiongea na blog ya bongo Xclusives Azma amefunguka
kuwa alipokuwa jijini mwanza mda mwingi aliutumia kufanya video za ngoma zake
zitakazopatikana kwenye album yake mpya itakayotoka hivi karibuni.
![]() |
| AZMA, BOB RAY KATIKA, NA VIDEO QUEEN |
“
Athma (Azma) attack ni shambulio la azma, nimejaribu kuzugumza vitu
vyenye ukweli ndani
yake juu sanaa yetu na maisha yetu wa ujumla, watu wategemee vitu
vikubwa kwenye
hii album ya video yenye ngoma kumi na nane (18), ni albam ya kwanza ya
hip hop afrika mashariki
ama afrika nzima kama sijakosea yenye video tupu, kuna wasanii wapo
kwenye game kwa mda mrefu lakini hawana hata video tano (5) kwa hiyo
this is a new attack”.
“msukumo wa kutoa album ya video ni kutokana na
nature ya mauzo ya album yangu ya kwanza, wateja wangu ambao kila nilipokuwa
nikipeleka album yangu ya love stories walikuwa wakiulizia video so niligundua
nikitoa album ya kuona italeta impact, kingine ni huu ulimwengu wa digital,
kuna sehemu zingine radio na tv za tanzania hazijafika huko… (nje ya nchi) so
niliona nikitoa album ya video itaweza kuwafikia kiurahisi na on time”.
Kwa zaidi ya asilimia themanini (80%) album ya “Athma
(Azma) Attack” video zimetengenezwa na Kinye media chini ya mwalim Kinye wa
Saut na director Bob ray ambae ni mdogo
wake Kinye na baadhi ya video zimefanywa na directors tofauti tofauti, kwa
upande wa audio kwa asilimia kubwa producer P. Mally wa Moss Records ndio kahusika,
na baadhi ya prodcers kama Double na D
classic wamechangia pia. Ngoma
zitakazopatikana kwenye hii album ni Mungu inusuru Tanzania, wanasubiri
nife, mama, Azma Attack, life is so hard feat Hard Mad, kuwa na athma,
Hip hop neno la uzima, mrs Azma feat Hard mad, chemsha bongo, nia moja
feat Rado, we never give up feat Dark Master n.k.
Kwa sasa Azma yuko jijini Dar es salaam akiendelea
kuuza album yake ya awali ya Love stories akiwa chini ya usimamizi wa
Tamadunimuzik.


0 comments:
Post a Comment