Baada ya kuachia Mixtape yake aliyopa jina la 'Utatu Mtakatifu' msanii
wa muziki wa kizazi kipya miondoko ya Hip Hop nchini, Webiro Wassira
'Wakazi' leo usiku anatarajia kuwasupries mashabiki wake kwa kuachia
nyimbo yake mpya ambayo haijajulikana ni wimbo gani.
Akizungumza na HOT SHOW kwa njia ya simu Wakazi alieleza kuwa anatarajia
kuachia nyimbo hiyo kama supries kwa mashabiki wake huku akikataa
kueleza jina la wimbo huo na sababu za kufanya hivyo.
Pamoja na hayo msanii huyo anatarajia kusafiri kwenda nchi ya mbali kwa
ajili ya kukamilisha mipango yake ya kuendeleza muziki wake kuweza
kuvuka mipaka ya nje ya Tanzania

0 comments:
Post a Comment