Maswali mengi bado yako mtaani kuhusu nini kinaendelea kwa upande wa Dayna kuhusu yale malalamiko yake kuwa ‘alipokonywa’ mdundo wa wimbo wake na ukatumika kufanya hit ya ‘My Number One’ ya Diamond Platinumz, ambapo alisema ameipeleka kesi COSOTA, wengi wanauliza ama ni vile alitaka kupata kick na kuipotezea? Ni maswali yaliyoko mtaani.
Mwimbaji huyo wa ‘Nivute Kwako’ ameiambia Hot show ya Highlands fm kile kinachoendelea na kwamba bado swala hilo liko COSOTA na yeye anaendelea kusubiria majibu, lakini anapata mrejesho kidogo kuhusu kile kinachoendelea japokuwa haruhusiwi kuyaongea.
Hata hivyo Dayna ameonesha hali ya kuwa na mashaka kidogo kwa kile kinachoendelea kutokana na mrejesho anaoupata, japokuwa hakuzungumza nini hasa kinampa kigugumizi, lakini sentensi zake zinatoa picha
.
“Mambo yetu yamekuwa na process kidogo, japo si kubwa sana, lakini tuombe Mungu..Mungu anaweza akajaalia muda wowote tukafikia muafaka, kwa sababu kwa upande wangu ninachosubiri ni maelezo tu, niitwe labda niambiwe kuna hiki na hiki.” Amesema Dayna.
0 comments:
Post a Comment