Nikki wa II aeleza kuwa wapo kwenye harakati za kumrudisha Lord Eyes ndani ya kampuni ya WEUSI

Msanii Nikki wa Pili kutoka katika kundi la muziki wa Hip hop Weusi ambao masikani yao ni jijini Arusha ameweka wazi kuwa siku za karibuni itafahamika hatima ya Msanii Lord Eyes ambaye awali alilipotiwa kuondolewa katika kundi hilo,Nikki aliweka wazi hilo alipokuwa akichat Live  katika ukurasa wa Facebook wa EATV katika kipengele cha Kikaangoni Live kinachokukutanisha na mtu maarufu

Moja ya maswali ambayo yameeulizwa sana na mashabiki kwa Nikki wa Pili ni kuhusu hatima ya msaniii Lord Eyes ambae alitimuliwa katika kundi hilo,hivyo msemaji wa weusi kampuni Nikki wa Pili akafunguka na kusema kuwa siku za karibuni msaniii huyo atarudi Weusi na kuendeleza harakati za muziki kwani amedai kuwa weusi ni kampuni inayoundwa na watu watano kwa mujibu wa sheria akiwemo Lord Eyes.

"Lord Eyes soon atarudi weusi maana sisi kama weusi kwa pamoja ni kampuni,hivyo weusi ni mtu 5 kama memorandam ya kampuni inavyo sema"  mbali na kuzungumzia kundi na hatima ya Lord Eyes Nikki amefungua siri nyingine kuwa kuna ngoma nyingine wamefanya na mwanamuziki bora wa Hip Hop kwa mwaka 2014 ambaye ni Fid Q na kudai kuwa kazi hiyo mpaka sasa bado hawajaitambulisha na waliifanya toka mwaka jana hivyo wakati utakapofika wataitoa ngoma hiyo.

Akiweka wazi mipango ya weusi kutoka Nikki amedai kuwa baada ya yeye kutambulisha na kupokelewa vizuri na ngoma ya sitaki kazi,wimbo mwingine utakaofuata utakuwa wa mkali Joh Makini.
Nikki wa pili akuacha kutoa somo kwa baadhi ya wasanii wa bongo ambao wamekuwa wakiipuuza Elimu na kukimbilia kufanya muziki na ujumbe wake kwao ni kuwa Elimu haina mbadala na kusoma ni kuchagua kuishi ukiwa na uhuru na ishara ya kustarabika katika jamii.

"Elimu haina mbadala...kusoma ni kuchaguwa kuishi huru na ku staarabika"  MSANII ANAEMKUBALI Nikki wa Pili amesema kuwa katika maisha yake yote amekuwa akitamani namna Jay Z alivyoishi maana alitoka katika maisha magumu na kubadili maisha yake hayo na kuwa mfano wa kuigwa katika mambo mengi,na amesababisha watu wengi kuamini kuwa historia ya maisha yao haiwafanyi kushindwa maisha.
"Namkubali sana Jay z..kaipeleka hip hop ikulu, na katika level za juu kibiashara,,pia ametuaminisha tulio kulia katika umaskini kuwa unaweza kuwa mtu yoyote historia yako haijalishi"
Nikki wa Pili ni msanii ambae kwa sasa anatamba na wimbo wake wa sitaki kazi,ambao ameamua kuihamasisha jamii hususani vijana kuacha dhana ya kutaka kuajiriwa bali wanaweza wenyewe kutafuta njia nyingine na kuweza kujiajiri wenyewe na kutengeneza ajira kwa watu wengine jambo ambalo baadae linaweza kuja zalisha mahitaji makubwa ya kazi
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment